Ulivyo Kiazi zaidi unaona sibu hazitoshi, unamtumia picha za uchi huyo mwanaume, tena wakati mwingine kwakua kichwani kuna funza unamtumia mke wako mapicha ya uchi ukiwa na mume wake kumuumiza Roho. Kwanza kabisa unatakiwa kujua kuwa huna jipya, umefukunyuliwa tu na usidhani kuwa labda wewe ni wakwanza una uspesho wowote, hapana mpo wengi tu unajidhalilisha bure.
Lakini pili unatakiwa kujua kuwa huyo si mume wako, picha ukishatuma basi ndiyo umetuma. Ukikutana na mwanake kauzu wala hahanagiki na wewe, anazichukua zile picha anaenda kuziprinti na baada ya wiki anazituma posta kwa Baba yako, ofisini na kama ni kauzu zaidi anatafuta tu lianaunti feki anazirusha kwenye mitandao unaishia kudhalilika.
Mwingine anasubiri umeachana na mume wake, umepata mwanaume anataka kukuoa, anazituma kwenye group la kamati ya maandalizi ya harusi siku mbili kabla hujaolewa. Mwingine anasubiri ushaolewa anamtumia mume wako analalamika kuwa unatembea na mume wake unamtumia picha za uchi? Kwakifupi kuna namna nyingi ambazo anaweza kukudhalilisha hivyo acha kuwa kiazi!
Unachepuka sawa, hakuna hata kipya unachokipata, tena basi ukiona mwanaume anachepuka halafu anaruhusu mchepuko kumpigia simu saa nane usiku, anaruhusu mchepuko kumtukana mke wake, ujue hajiamini. Kama huyo mwanaume halelewi na mke wake, kwa maana ya hiyo Boxer anayovaa sio kanunuliwa na mke wake basi hana nguvu za kiume ni dakika mbili chali, hajiamini hana amani ndiyo maana anataka kuonekana kidume.
Ukiona Povu hili ujue kuna mtu kaachwa kwasababu ya kijinga kama hii
Comments
Post a Comment