Skip to main content

JE NI POA KUPASHA KIPORO NA MPENZI WAKO WA ZAMANI

Hakuna dharau kubwa kwa mwanamke kama vile mwanaume ambaye alikua mpenzi wako halafu akaoa mwanamke mwingine halafu anarudi kwako anakuambia bado anakupenda anataka kufanya tena mapenzi na wewe. Hapa naamanisha bila kujali sababu za yeye kukuacha kama alikuacha na kwenda kuoa mwingine halafu bado anakutumia kingono basi jua kuwa sio kwamba anakupenda na anashindwa kukusahau hapana ni kwamba amekudharau na anakuona mpumbavu.

Hata kama alikuacha kwakua mmetofautiana Dini, hata kama alikatazwa na wazazi wake hata kama ni wewe ulimuacha, lakini kama mliachana na akarudi kutembea na wewe baada ya kuoa basi jua kuwa kakudharau. Kwanza kabisa anajua kabisa hujithamini ndiyo maana kwako anakua kimwili na kwa mkewe anaenda kutengeneza maisha. Lakini ni kama anajihakikishia kuwa huyu si mwanamke wa kuoa kabisa na alifanya maamuzi sahihi.

Iko hivi moja ya wanawake ambao wanaume huwadharau ni wanawake ambao wanatembea na waume za watu tena bila malengo. Lakini atakua amekuona mpuuzi kabisa kama wewe utakua umeolewa na mwanaume mwingine halafu ukarudiana na yeye, huyu mwanaume hatakuheshimu na kwani anajau kua huithamini ndoa yako.

Hata kama ikitokea ukaachika kwa mume wako basi jua kuwa kama livyokuacha mara ya kwanza na kuoa mwingine hatamuacha mkewe kwaajili yako. Hii ni kwasababu anajua kuwa wewe si mtu wa kuaminika ni kicheche. Wanaume tunapenda sana kusaliti lakini si kusalitiwa. Anajua kuwa kama ulimsaliti mumeo na X wako basi hata yeye unaweza kumsaliti na X wako hivyo ni vigumu sana kuendelea na mahusiano baada ya kuona umeachika.

Najua unadhani unamkomoa mke wake, tena kwakua anaonyesha kukujali kuliko mkewe, hata wakati mwingine kutumia muda mwingi na wewe na kumtukana au kumnyanyasa mbele yako ukafikiri wewe una thamani zaidi. Hapana anajifanya nikua anakuridhisha tu, anajua mkewe hawezi kuondoka hivyo ili kukushikilia wewe na kuendelea kukutumia nilazima aonyeshe kama vile anakujali wewe zaidi kuliko mkewe ili usiondoke!

Comments

Popular posts from this blog

MKUNDE PORI KIBOKO YA UZAZI | TASA

MIZIZI YA MKUNDE PORI NA FAIDA ZAKE ■ Inasafisha kizazi ■ Inazibua mirija iliyoziba ■ Inaondoa sumu kwa wale waliotumia sindano za uzazi/vidonge vya uzazi. ■ Inakomaza mayai kwa wale wenye tatizo la mayai kutokukomaa na kusababisha mayai kutokupevuka ■ Inasogeza kizazi karibu kwa wale ambao vizazi vyao vipo mbali ■ Majani ya mkunde pori pia ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume • Dalili mojawapo itakayokufanya ujue dawa hii ya mkunde pori inafanya kazi ni kwenda haja ndogo mara nyingi kuliko kawaida. • Dalili nyingine ni tumbo kuvuta sana chini ya kitovu. Usipoona dalili hizi usiogope maana ukubwa wa tatizo unatofautiana. ANGALIZO KWA WANAWAKE WATAKAOTUMIA KWA AJILI YA UZAZI, Ukinywa dawa hii hakikisha siku za hatari unakutana na mwenzi wako...na baada ya hapo usitumie dawa mpaka upime mimba kwanza maana mimba nyingine dalili zake huchelewa kuonekana hivyo unaweza ukanywa tena mimba kama imeingia ikatoka. Wajawazito hawaruhusiwi kutumia. MATUMIZ CHUKUA MIZIZ

RAHA YA KUWA NA MWANAMKE MWEUSI KWENYE MAHUSIANO

Nilikuwaga sielewi kwanini hawa wanawake weusi aka blacks wanasifiwa sana?. Jaman hii type ni raha sana kudate nayo unakuwa huna stress kwanza hawana vizinga vya kizembe zembe, wanaridhika hata wakipewa kitu kidogo, yani wanajua kupenda na wengi wana true love. Sijamaliza bado, wanawake weusi wanajua nini maana ya mapenzi, wanajua kukaa na mwanaume halafu pia wanajituma sana akija ghetto anafanya kila kitu hadi kubrash viatu.  Ukija kwenye kule kwa 6x6 sio wachoyo kukupa na wanajua balaa ni mafundi na hawana maringo kabisa.  Shida ya hizi rangi nyeupe ni kwamba zina maringo sana na wanavizinga sana unakuta dada kaupele kadogo kameota anataka dawa halafu utasikia 50k dawa ya uson wtf?? Hawa mademu weupe wana vizinga sana halafu wengi ni malaya sana. Nasema haya coz me nilikuwa mhanga sana wa hizi type nyeupe ila toka nianze kula hizi nyeusi mmeona utofauti mkubwa sana mpaka nimeanza kuwaelewa mablacks yani hawana complications. Popote mlipo nyie wanawake weusi agizeni mirinda

STORI YANGU; NILIZAA NA WEWE KWAKUA UNAWEZA KUHUDUMIA MTOTO!

Wote tuliingia kazini siku moja, mimi niliajiriwa kama afisa mikopo wakati yeye aliajiriwa kama mhasibu lakini wote tulianzia kama mateila mpaka baada ya kama miezi sita hivi ndiyo tulitoka na kila mtu akawa ameenda katika kitengo chake.  Kuna dada mwingine ambaye walikua kitengo komoja na wote tulikua marafiki. Mimi ni msiri sana hivyo hata nilipoanzisha mahusiano yangu na Kelvin (Sio jina lake halisi) sikumuambia mtu yoyote zaidi ya Edna ambaye ingawa tulikutana kazini lakini alishaanza kuwa kama Dada yangu. Edna alikua ni rafiki yangu mkubwa, anakuja nyumbani kwangu tunaongea na nilimsaidia katika mambo mengi. Wakati Mama yake anaumwa kalazwa hospitali nakumbuka aliishiwa kabisa, hata kodi ya nyumba alikosa, walitaka kumfukuza lakini nikatoa pesa yangu laki tisa na kumlipia, baadaye alipotaka kunirudishia nilimuambia hapana. Alishukuru sana, kwa upande wa Kelvin mahusiano yetu yalikua hatakaharaka, tulifanya karibu kila kitu pamoja. Wakati nanunua kiwanja ili kujenga yeye ali