Kama upo kwenye mahusiano na mwanaume miaka mitatu na haeleweki basi ukimaliza kusoma hapa muulize sio kwa kulalamika, kwa kumuangalia usoni muulize hivi una mpango wa kunioa au unanipotezea muda wangu tu. Acha kudhani kwakua anakuambia anakupenda atakuoa, acha kudhani kwakua amekuambia mfungue biashjara ya pamoja atakuoa, acha kudhani kwakua amekuambia umzalie atakuoa, acha kudhani kwakua mnaishi pamoja atakuoa, acha kudhani kwakua ulimtafutia kazi atakuooa.
Acha kudhani kwakua ndugu zake wanakujua anakuacha uongee na Mama yake atakuoa. Acha kudhani kwakua anakusifia kua wewe ni wife material atakuoa. Muulize tena acheni lile swali la “Kwetu utakuja lini kujitambulisha?” Ndugu yangu aje kwanu kakuambia anakutaka, au alishaweka ahadi muulize uso mkavu kama umepiga cha arusha “Hivi una mpango wa kunioa au huna?” inawezekana hajafikia kuoa lakini ana mpango na wewe au amefikia lakini hana mpango na wewe.
Miaka mitatu ni mingi kwa mtu kukuchunguza tabia, labda kama anataka kujua na maini yako yaje au kuchunguza namna utumbo wako ulivyojinyongorokota! Ila nataka mnielewe, miaka mitatu haihusu mapenzi ya utoto kipindi mko sekondari au chuo,. Miaka mitatu haihuishi kipindi ambacho mwanaume kamaliza chuo hana kazi. Hapana, miaka mitatu haihusu wale ambao mnatembea na vivulana, vina miaka 30 lakini vipo kwao na havina mpango hata wakuondoka.
Ukitaka kuhesabu miaka mitatu angalia miaka ambayo kamaliza chuo, kapata kazi, kaakaa miaka miwili kazini kisha hesabu mitatu baada ya yeye kupata kazi na kuwa mwanaume. Sio mtu hana kazi hata kama mko naye miaka kumi unataka akuoe, akupeleke wapi? Kwanza mwanaume akiwa bado hajapata pesa huwezi jua hata anakupenda, inawezekana hata yuko na wewe kwakua ana shida tu akipata pesa anamfuata yule dada mwingine sijui nani halafu unaulizia akuoe lini?
Hii pia haiwahusu wale wadada ambao mnafanya kazi lakini badala ya kusaidia ndugu zenu mmechukua mwanaume mtu mzima mmemuweka ndani mnamhudumia, nyie subirini kuiachika akishapata pesa! Unataka akuoe nini wakati ushamuoa? Unamhudumia mwanaume kila kitu halafu unataka akuoe? Yaani mtu ambaye hata yeye mwenyewe hawezi kujihudumia unataka aoe ili? Unajua anaandika sana , sijui kama mmenielewa, ila kama haeleweki miaka mitatu basi hataeleweka kumi, sisemi hatakuoa lakini ishi kwa tahadhari usijiozeshe kisa mmeishi sita ukaanza kumuita mume!
Najua inaume kwakua ulishawekeza nguvu nyingi sana kwake ila sasa mimi nifanyeje, hamna namna fuatilia blog yangu kila siku kufahamu mengi zaidi
Acha kudhani kwakua ndugu zake wanakujua anakuacha uongee na Mama yake atakuoa. Acha kudhani kwakua anakusifia kua wewe ni wife material atakuoa. Muulize tena acheni lile swali la “Kwetu utakuja lini kujitambulisha?” Ndugu yangu aje kwanu kakuambia anakutaka, au alishaweka ahadi muulize uso mkavu kama umepiga cha arusha “Hivi una mpango wa kunioa au huna?” inawezekana hajafikia kuoa lakini ana mpango na wewe au amefikia lakini hana mpango na wewe.
Miaka mitatu ni mingi kwa mtu kukuchunguza tabia, labda kama anataka kujua na maini yako yaje au kuchunguza namna utumbo wako ulivyojinyongorokota! Ila nataka mnielewe, miaka mitatu haihusu mapenzi ya utoto kipindi mko sekondari au chuo,. Miaka mitatu haihuishi kipindi ambacho mwanaume kamaliza chuo hana kazi. Hapana, miaka mitatu haihusu wale ambao mnatembea na vivulana, vina miaka 30 lakini vipo kwao na havina mpango hata wakuondoka.
Ukitaka kuhesabu miaka mitatu angalia miaka ambayo kamaliza chuo, kapata kazi, kaakaa miaka miwili kazini kisha hesabu mitatu baada ya yeye kupata kazi na kuwa mwanaume. Sio mtu hana kazi hata kama mko naye miaka kumi unataka akuoe, akupeleke wapi? Kwanza mwanaume akiwa bado hajapata pesa huwezi jua hata anakupenda, inawezekana hata yuko na wewe kwakua ana shida tu akipata pesa anamfuata yule dada mwingine sijui nani halafu unaulizia akuoe lini?
Hii pia haiwahusu wale wadada ambao mnafanya kazi lakini badala ya kusaidia ndugu zenu mmechukua mwanaume mtu mzima mmemuweka ndani mnamhudumia, nyie subirini kuiachika akishapata pesa! Unataka akuoe nini wakati ushamuoa? Unamhudumia mwanaume kila kitu halafu unataka akuoe? Yaani mtu ambaye hata yeye mwenyewe hawezi kujihudumia unataka aoe ili? Unajua anaandika sana , sijui kama mmenielewa, ila kama haeleweki miaka mitatu basi hataeleweka kumi, sisemi hatakuoa lakini ishi kwa tahadhari usijiozeshe kisa mmeishi sita ukaanza kumuita mume!
Najua inaume kwakua ulishawekeza nguvu nyingi sana kwake ila sasa mimi nifanyeje, hamna namna fuatilia blog yangu kila siku kufahamu mengi zaidi
Comments
Post a Comment