Wote tulikua tunaona mambo aliyokua anafanya Kaka yetu, si kwamba hatukua tunaweza kumuambia hapana, ni kama kila mtu alikua akimchukia mke wake ingawa hatukuwa na sababu yoyote. Mara kadhaa Mama alienda na kumtukana lakini wifi alivumilia na hakusema chochote. Kaka yangu alikua akimpelekea wanawake mpaka ndani lakini wifi alivumilia, mimi nilikua naishi kwa Kaka na niliona na kuumia.
Mara kadhaa alipochoka na kutaka kuondoka Kaka alimuambia aondoke lakini amuachie wanae. Mungu aliwabariki watoto watatu, wakike wawili na wakiume mmoja, wifi alivumilia na kukubali kuteseka kwaajili ya wanae. Kipindi hicho mimi nilikua darasa la saba hivyo kidogo nilikua napatana na wifi kwani kweli sikuwahi kumuona na kosa lolote na nilishangaa ni kwa namna gani ndugu zangu wengine walikua wanamchukia.
Siku moja nilikua nimatoka shule nakumbuka ndiyo nilitoka kufanya mtihani wa taifa kumaliza darasa la saba. Nilipofika nyumbani kwa Kaka ambapo mimi nilikua nikiishi nilikuta kuna watu wengi wamejaa. Kwa kuangalia tu nilistua kwani ilionekana kama msiba, nilitembea kwa harakaharaka na kufika pale. Nilimuona Mama amezimia na Kaka anapepewa analia kama mtoto mdogo, nilianza kuwaza ni nani kafariki wanalia hivyo.
Hakuna mtu aliyeniambia chochote, nilianza kuuliza na kuuliza ndipo nilipopatiwa habari. Watoto wote wa Kaka yangu walikua wamefariki, nilishindwa kuelewa sikutaka kuamini, niliendelea kuuliza nini kilikua kimetokea ndipo Dada yangu ninayemfuatia alinionyesha Barua. Kuona tu nilijua muandiko, ulikua ni wa mtoto wa kwanza wa Kaka yangu ambaye alikua ni kama mdogo wangu. Alikua na miaka 12, siku hiyo haikua siku ya shule kwao kwani sisi tulikua tunafanya mtihani wa Taifa, iliandikwa.
“Kwako Mama, Sikamoo. Tunakuandikia hii barua kwakua tunakupenda sana, mimi na wadogo zangu tumeona namna unvayoteseka kwaajili yetu. Baba anakupiga na kukunyanyasa kila siku, tunajua umechoka na unataka kuondoka lakini kwakua unaogopa Baba atatutesa basi umeamua kubaki. Sisi tumeamua kuondoka ili wewe uishi vizuri, sisi tunaenda sehemu nzuri kukusubiri.
Mama tunashukuru kwa kutulinda miaka yote hiyo lakini kama tukikuacha na Baba basi atakuua na sisi hatutapata tena Mama kama wewe. Hatutaki kulelewa na Mama wa Kambo. Mama usilie kwani ukiamka asubuhi sisi tutakua tumelala, usijali Mama huko kwa Mungu tutakua salama, mimi nitawalinda wadogo zangu, usiogope tena unaweza kuondoka sasa kwani Baba hatakutishia tena, sisi hawezi kutudhuru. Kwa heri Mama tunaomba umuache Baba.”
Barua ile ilishia hapo, watoto wa Kaka walikaa na kuona kuwa njia pekee ya kumuokoa Mama yao na mateso ya Kaka ni kwa wao kunywa sumu. Walinunua sumu ya Panya mjini na kuweka kwenyeJuice wote wakanywa usiku na asubuhi walikua wamekwisha fariki, mmoja alikua na miaka 13, 9 na wa mwisho miaka 6. Hakuna liyetaka kuamini lakini ilikua ni kweli, Kaka alipoteza watoto wake wote kwaajili ya kumnyanyasa mke wake.
Siku ile kila mtu alimuangalia Kaka kama shetani, wifi alilia na kulia na kila wakati alijilaumu ni kwanini hakuchukua hatua. Ni kwanini hakutoroka na watoto wake au hata hakwenda Polisi. Baada ya mazishi aliondoka na kurudi kwao, Kaka alibaki mpweke na wiki mbili tu baada ya mazishi ya wanae kutokana na msongo wa mawazo Kaka alijipiga risasi na kufa.
Ni miaka ziadi ya kumi imepita lakini mpaka leo familia yetu haiko sawa, Mama yangu amekua kama chizi, ndugu zangu wengine nao hakuna mwenye ndoa ya maana, mimi ndiyo nimaliza chuo, lakini sina hata mpenzi. Kila siku nimekua nikijilaumu kutokana na hili tukio nikiamini labda ningefanya kitu mambo yangekua tofauti. Nimeamua kukiandika labda na mimi nitapata nafuu ya maisha kwani sina furaha sina amani katika moyo wangu.
****MWISHO
Mara kadhaa alipochoka na kutaka kuondoka Kaka alimuambia aondoke lakini amuachie wanae. Mungu aliwabariki watoto watatu, wakike wawili na wakiume mmoja, wifi alivumilia na kukubali kuteseka kwaajili ya wanae. Kipindi hicho mimi nilikua darasa la saba hivyo kidogo nilikua napatana na wifi kwani kweli sikuwahi kumuona na kosa lolote na nilishangaa ni kwa namna gani ndugu zangu wengine walikua wanamchukia.
Siku moja nilikua nimatoka shule nakumbuka ndiyo nilitoka kufanya mtihani wa taifa kumaliza darasa la saba. Nilipofika nyumbani kwa Kaka ambapo mimi nilikua nikiishi nilikuta kuna watu wengi wamejaa. Kwa kuangalia tu nilistua kwani ilionekana kama msiba, nilitembea kwa harakaharaka na kufika pale. Nilimuona Mama amezimia na Kaka anapepewa analia kama mtoto mdogo, nilianza kuwaza ni nani kafariki wanalia hivyo.
Hakuna mtu aliyeniambia chochote, nilianza kuuliza na kuuliza ndipo nilipopatiwa habari. Watoto wote wa Kaka yangu walikua wamefariki, nilishindwa kuelewa sikutaka kuamini, niliendelea kuuliza nini kilikua kimetokea ndipo Dada yangu ninayemfuatia alinionyesha Barua. Kuona tu nilijua muandiko, ulikua ni wa mtoto wa kwanza wa Kaka yangu ambaye alikua ni kama mdogo wangu. Alikua na miaka 12, siku hiyo haikua siku ya shule kwao kwani sisi tulikua tunafanya mtihani wa Taifa, iliandikwa.
“Kwako Mama, Sikamoo. Tunakuandikia hii barua kwakua tunakupenda sana, mimi na wadogo zangu tumeona namna unvayoteseka kwaajili yetu. Baba anakupiga na kukunyanyasa kila siku, tunajua umechoka na unataka kuondoka lakini kwakua unaogopa Baba atatutesa basi umeamua kubaki. Sisi tumeamua kuondoka ili wewe uishi vizuri, sisi tunaenda sehemu nzuri kukusubiri.
Mama tunashukuru kwa kutulinda miaka yote hiyo lakini kama tukikuacha na Baba basi atakuua na sisi hatutapata tena Mama kama wewe. Hatutaki kulelewa na Mama wa Kambo. Mama usilie kwani ukiamka asubuhi sisi tutakua tumelala, usijali Mama huko kwa Mungu tutakua salama, mimi nitawalinda wadogo zangu, usiogope tena unaweza kuondoka sasa kwani Baba hatakutishia tena, sisi hawezi kutudhuru. Kwa heri Mama tunaomba umuache Baba.”
Barua ile ilishia hapo, watoto wa Kaka walikaa na kuona kuwa njia pekee ya kumuokoa Mama yao na mateso ya Kaka ni kwa wao kunywa sumu. Walinunua sumu ya Panya mjini na kuweka kwenyeJuice wote wakanywa usiku na asubuhi walikua wamekwisha fariki, mmoja alikua na miaka 13, 9 na wa mwisho miaka 6. Hakuna liyetaka kuamini lakini ilikua ni kweli, Kaka alipoteza watoto wake wote kwaajili ya kumnyanyasa mke wake.
Siku ile kila mtu alimuangalia Kaka kama shetani, wifi alilia na kulia na kila wakati alijilaumu ni kwanini hakuchukua hatua. Ni kwanini hakutoroka na watoto wake au hata hakwenda Polisi. Baada ya mazishi aliondoka na kurudi kwao, Kaka alibaki mpweke na wiki mbili tu baada ya mazishi ya wanae kutokana na msongo wa mawazo Kaka alijipiga risasi na kufa.
Ni miaka ziadi ya kumi imepita lakini mpaka leo familia yetu haiko sawa, Mama yangu amekua kama chizi, ndugu zangu wengine nao hakuna mwenye ndoa ya maana, mimi ndiyo nimaliza chuo, lakini sina hata mpenzi. Kila siku nimekua nikijilaumu kutokana na hili tukio nikiamini labda ningefanya kitu mambo yangekua tofauti. Nimeamua kukiandika labda na mimi nitapata nafuu ya maisha kwani sina furaha sina amani katika moyo wangu.
****MWISHO
Comments
Post a Comment