Skip to main content

SIMULIZI; MAMA USILIE KWANI UKIAMKA ASUBUHI SISI TUTAKUA TUMELALA!

Wote tulikua tunaona mambo aliyokua anafanya Kaka yetu, si kwamba hatukua tunaweza kumuambia hapana, ni kama kila mtu alikua akimchukia mke wake ingawa hatukuwa na sababu yoyote. Mara kadhaa Mama alienda na kumtukana lakini wifi alivumilia na hakusema chochote. Kaka yangu alikua akimpelekea wanawake mpaka ndani lakini wifi alivumilia, mimi nilikua naishi kwa Kaka na niliona na kuumia.

Mara kadhaa alipochoka na kutaka kuondoka Kaka alimuambia aondoke lakini amuachie wanae. Mungu aliwabariki watoto watatu, wakike wawili na wakiume mmoja, wifi alivumilia na kukubali kuteseka kwaajili ya wanae. Kipindi hicho mimi nilikua darasa la saba hivyo kidogo nilikua napatana na wifi kwani kweli sikuwahi kumuona na kosa lolote na nilishangaa ni kwa namna gani ndugu zangu wengine walikua wanamchukia.

Siku moja nilikua nimatoka shule nakumbuka ndiyo nilitoka kufanya mtihani wa taifa kumaliza darasa la saba. Nilipofika nyumbani kwa Kaka ambapo mimi nilikua nikiishi nilikuta kuna watu wengi wamejaa. Kwa kuangalia tu nilistua kwani ilionekana kama msiba, nilitembea kwa harakaharaka na kufika pale. Nilimuona Mama amezimia na Kaka anapepewa analia kama mtoto mdogo, nilianza kuwaza ni nani kafariki wanalia hivyo.

Hakuna mtu aliyeniambia chochote, nilianza kuuliza na kuuliza ndipo nilipopatiwa habari. Watoto wote wa Kaka yangu walikua wamefariki, nilishindwa kuelewa sikutaka kuamini, niliendelea kuuliza nini kilikua kimetokea ndipo Dada yangu ninayemfuatia alinionyesha Barua. Kuona tu nilijua muandiko, ulikua ni wa mtoto wa kwanza wa Kaka yangu ambaye alikua ni kama mdogo wangu. Alikua na miaka 12, siku hiyo haikua siku ya shule kwao kwani sisi tulikua tunafanya mtihani wa Taifa, iliandikwa.

“Kwako Mama, Sikamoo. Tunakuandikia hii barua kwakua tunakupenda sana, mimi na wadogo zangu tumeona namna unvayoteseka kwaajili yetu. Baba anakupiga na kukunyanyasa kila siku, tunajua umechoka na unataka kuondoka lakini kwakua unaogopa Baba atatutesa basi umeamua kubaki. Sisi tumeamua kuondoka ili wewe uishi vizuri, sisi tunaenda sehemu nzuri kukusubiri.

Mama tunashukuru kwa kutulinda miaka yote hiyo lakini kama tukikuacha na Baba basi atakuua na sisi hatutapata tena Mama kama wewe. Hatutaki kulelewa na Mama wa Kambo. Mama usilie kwani ukiamka asubuhi sisi tutakua tumelala, usijali Mama huko kwa Mungu tutakua salama, mimi nitawalinda wadogo zangu, usiogope tena unaweza kuondoka sasa kwani Baba hatakutishia tena, sisi hawezi kutudhuru. Kwa heri Mama tunaomba umuache Baba.”

Barua ile ilishia hapo, watoto wa Kaka walikaa na kuona kuwa njia pekee ya kumuokoa Mama yao na mateso ya Kaka ni kwa wao kunywa sumu. Walinunua sumu ya Panya mjini na kuweka kwenyeJuice wote wakanywa usiku na asubuhi walikua wamekwisha fariki, mmoja alikua na miaka 13, 9 na wa mwisho miaka 6. Hakuna liyetaka kuamini lakini ilikua ni kweli, Kaka alipoteza watoto wake wote kwaajili ya kumnyanyasa mke wake.

Siku ile kila mtu alimuangalia Kaka kama shetani, wifi alilia na kulia na kila wakati alijilaumu ni kwanini hakuchukua hatua. Ni kwanini hakutoroka na watoto wake au hata hakwenda Polisi. Baada ya mazishi aliondoka na kurudi kwao, Kaka alibaki mpweke na wiki mbili tu baada ya mazishi ya wanae kutokana na msongo wa mawazo Kaka alijipiga risasi na kufa.

Ni miaka ziadi ya kumi imepita lakini mpaka leo familia yetu haiko sawa, Mama yangu amekua kama chizi, ndugu zangu wengine nao hakuna mwenye ndoa ya maana, mimi ndiyo nimaliza chuo, lakini sina hata mpenzi. Kila siku nimekua nikijilaumu kutokana na hili tukio nikiamini labda ningefanya kitu mambo yangekua tofauti. Nimeamua kukiandika labda na mimi nitapata nafuu ya maisha kwani sina furaha sina amani katika moyo wangu.

****MWISHO

Comments

Popular posts from this blog

MKUNDE PORI KIBOKO YA UZAZI | TASA

MIZIZI YA MKUNDE PORI NA FAIDA ZAKE ■ Inasafisha kizazi ■ Inazibua mirija iliyoziba ■ Inaondoa sumu kwa wale waliotumia sindano za uzazi/vidonge vya uzazi. ■ Inakomaza mayai kwa wale wenye tatizo la mayai kutokukomaa na kusababisha mayai kutokupevuka ■ Inasogeza kizazi karibu kwa wale ambao vizazi vyao vipo mbali ■ Majani ya mkunde pori pia ni dawa ya kuongeza nguvu za kiume • Dalili mojawapo itakayokufanya ujue dawa hii ya mkunde pori inafanya kazi ni kwenda haja ndogo mara nyingi kuliko kawaida. • Dalili nyingine ni tumbo kuvuta sana chini ya kitovu. Usipoona dalili hizi usiogope maana ukubwa wa tatizo unatofautiana. ANGALIZO KWA WANAWAKE WATAKAOTUMIA KWA AJILI YA UZAZI, Ukinywa dawa hii hakikisha siku za hatari unakutana na mwenzi wako...na baada ya hapo usitumie dawa mpaka upime mimba kwanza maana mimba nyingine dalili zake huchelewa kuonekana hivyo unaweza ukanywa tena mimba kama imeingia ikatoka. Wajawazito hawaruhusiwi kutumia. MATUMIZ CHUKUA MIZIZ

RAHA YA KUWA NA MWANAMKE MWEUSI KWENYE MAHUSIANO

Nilikuwaga sielewi kwanini hawa wanawake weusi aka blacks wanasifiwa sana?. Jaman hii type ni raha sana kudate nayo unakuwa huna stress kwanza hawana vizinga vya kizembe zembe, wanaridhika hata wakipewa kitu kidogo, yani wanajua kupenda na wengi wana true love. Sijamaliza bado, wanawake weusi wanajua nini maana ya mapenzi, wanajua kukaa na mwanaume halafu pia wanajituma sana akija ghetto anafanya kila kitu hadi kubrash viatu.  Ukija kwenye kule kwa 6x6 sio wachoyo kukupa na wanajua balaa ni mafundi na hawana maringo kabisa.  Shida ya hizi rangi nyeupe ni kwamba zina maringo sana na wanavizinga sana unakuta dada kaupele kadogo kameota anataka dawa halafu utasikia 50k dawa ya uson wtf?? Hawa mademu weupe wana vizinga sana halafu wengi ni malaya sana. Nasema haya coz me nilikuwa mhanga sana wa hizi type nyeupe ila toka nianze kula hizi nyeusi mmeona utofauti mkubwa sana mpaka nimeanza kuwaelewa mablacks yani hawana complications. Popote mlipo nyie wanawake weusi agizeni mirinda

STORI YANGU; NILIZAA NA WEWE KWAKUA UNAWEZA KUHUDUMIA MTOTO!

Wote tuliingia kazini siku moja, mimi niliajiriwa kama afisa mikopo wakati yeye aliajiriwa kama mhasibu lakini wote tulianzia kama mateila mpaka baada ya kama miezi sita hivi ndiyo tulitoka na kila mtu akawa ameenda katika kitengo chake.  Kuna dada mwingine ambaye walikua kitengo komoja na wote tulikua marafiki. Mimi ni msiri sana hivyo hata nilipoanzisha mahusiano yangu na Kelvin (Sio jina lake halisi) sikumuambia mtu yoyote zaidi ya Edna ambaye ingawa tulikutana kazini lakini alishaanza kuwa kama Dada yangu. Edna alikua ni rafiki yangu mkubwa, anakuja nyumbani kwangu tunaongea na nilimsaidia katika mambo mengi. Wakati Mama yake anaumwa kalazwa hospitali nakumbuka aliishiwa kabisa, hata kodi ya nyumba alikosa, walitaka kumfukuza lakini nikatoa pesa yangu laki tisa na kumlipia, baadaye alipotaka kunirudishia nilimuambia hapana. Alishukuru sana, kwa upande wa Kelvin mahusiano yetu yalikua hatakaharaka, tulifanya karibu kila kitu pamoja. Wakati nanunua kiwanja ili kujenga yeye ali