Mapenzi ya Mama kwa mtoto wake ni ya kipekee ambayo hayawezi kufananishwa na kitu chochote, narudia hayawezi kufananishwa na mapenzi ya aina yoyote hata yale ya Baba kwa mtoto wake.
Hii ndiyo maana mwili wa mwanamke bila kujijua unamlinda mtoto tangu siku ya kwanza ya kutungwa mimba. Kuna mambo ambayo wanawake hufanya bila kujijua wanafanya nini lakini ni ya muhimu sana kwa maisha ya watoto wao.
Nadhani umeshawahi kuona, mtoto akiwa mchanga, akinamama hupenda kuwabusubusu, Mama atambusu mtoto kila mara, akamkumbatia na hata kutamani kumng’ata.
Kama ni Mama nadhani unajua, unaweza kujikuta unambusu tu mwanao, wakati mwingine bila hata kujali ni mchafu au la? Hivi unajua kuwa ni kwanini?
Lakini Mama unakuta anamng’ata kucha mtoto, yaani kamshika na wala hajali anang’ata moja moja, yeye anadhani ni kwakua anaogopa wembe utamkata, hapana kuna kitu kingine zaidi ya hicho!
Lakini pia unakumbuka kuwa, kuna siku uji ulimwagikia mwanao mkononi badala ya kumfuta kwa kitambaa ukaulamba ule mkono? Hivi unajua kwanini ulifanya hivyo?
Najua unadhani kuwa ni kwaajili ya mapezni uliyonayo kwake, nikweli lakini kuna kitu kingine kikubwa zaidi ha hicho. Kinga ya mtoto kwa magonjwa hutengenezwa wakati mtoto yuko tumboni.
Lakini hiyo ni kidogo sana na haitoshi, kwani mtoto anakua yuko sehemu salama, mtoto anapozaliw ana kukutana na mzingira ya nnje, kunakuwa na uchafu, wadudu na vitu vingine ambavyo vinaweza kumsafishia magonjwa wkaati hana kinga ya kutosha.
Sasa Mama anapombusu mtoto wake, anapomng’ata kucha, kumlamba mikono, ni mwili wake unamuambia kufanya hivyo. Mdomo wa Mama unapogusa mwili wa mtoto, kunakuwa na wadudu wadudu wa ambao husababusha magonjwa.
Sasa mwili wa Mama unachukua sample ya wale wadudu, kupitia mdomo, pua na kupeleka mwilini kwa Mama. Unauambia mwili wa Mama kuwa mwanao kazungukwa na wadudu flani na flani.
Mwili wa Mama unatengeneza kinga kwaajili ya wale wadudu ambao mtoto anaweza kuwameza kwa kushika, kula, au kupumua. Sasa ile kinga hupelekwa katika maziwa ya Mama.
Mtoto anaponyonya basi anakutana na kinga ile tayari ishatengenezwa. Ndiyo Mama anamtengenezea mwanae dawa, hii ndiyo maana unashauriwa kunyonyesha kwa muda mrefu kwani wakati huo mwili wa mtoto haujawa imara sana kutengeneza kinga yake wenyewe.
Sasa kwanini usimpende Mama yako wakati ndiyo alikua Daktari wako wa kwanza, ndiyo inawezekana ana mapungufu yake kama mwanadamu lakini hembu pima mazuri aliyokufanyia na hayo unayoyaona mabaya.
Comments
Post a Comment